![](https://static.wixstatic.com/media/84f169_23a385117d4e4025b86251b252e5bab7~mv2.png/v1/fill/w_940,h_788,al_c,q_90,enc_avif,quality_auto/84f169_23a385117d4e4025b86251b252e5bab7~mv2.png)
Rais wa shirikisho la soka duniani (FIFA) Gianni Infantino ametolea uvivu sakata la mashabiki wanozungumza na kulalamika sana juu ya ukatazwaji wa pombe katika kombe la dunia nchini Qatar.
Infantino amesema haoni sababu ya msingi watu kutoa malalamiko hayo kwani kukosa pombe kwa masaa kadhaa haiwezi kumuathiri mtu na hali hii inatokea hata kwa baadhi ya mataifa ya ulaya ambapo watu huzuiwa kunywa pombe kwa masaa kadhaa.
"kama pombe ni tatizo basi nitajiuzulu na kwenda kupumzika ufukweni" alinukuliwa rais huyo wa FIFA.
Comments